JamiiAsia
Indonesia yasimamisha uokoaji baada ya volkano kuripuka tena
4 Desemba 2023Matangazo
Hapo awali miili ya wapanda mlima 11 ilipatikana wakati wa kuwatafuta waliopotea lakini juhudi za kuwaondoa zilishindikana kutokana na kuripuka tena kwa mlima huo.
Mkuu wa Idara ya Ukoaji, Abdul Malik, alisema zoezi hilo lingeendelea hali itakapotengemaa.
Mlima wa Marapi uliripuka siku ya Jumapili (Disemba 3) na kutoa majivu ya moto.
Soma zaidi: Vifo Indonesia kufuatia mripuko wa volkano sasa ni 34
Mlima huo umewekwa katika kiwango cha juu cha tahadhari tangu mwaka 2011 na hivyo kuwapiga marufuku wanaofanya shughuli za kuupanda.
Wapanda milima stadi 75 walianza kuupanda mlima huo siku ya Jumamosi na kufikia juu karibu mita 2,900 ambako walikwama.