1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Kwa mwaka uliopita Iran imewanyonga watu 834

Sylvia Mwehozi
5 Machi 2024

Mashirika mawili ya kutetea haki za binadamu yamesema kuwa Iran iliwanyonga watu wasiopungua 834 mwaka jana, ikiwa ni idadi kubwa zaidi tangu mwaka 2015 huku adhabu ya kifo ikizidi kuongezeka katika taifa hilo.

Israeli | Maandamano ya kutetea haki za wanawake nchini Iran
Maandamano ya kutetea haki za wanawake nchini Iran - Septemba 16, 2023, Madrid, Uhispania: Mwandamanaji wa Iran akiwa ameshikilia bango lenye uso wa Mahsa Amini wakati wa maandamano hayo.Picha: David Canales/SOPA Images/picture alliance

Taarifa hiyo imetolewa na shirika la haki za binadamu lenye makao yake makuu Norway na jingine la mjini Paris. Mashirika hayo yamesema idadi ya watu walionyongwa, kwa Iran kutekeleza adhabu hiyo katika miaka ya hivi karibuni, iliongezeka kwa asilimia 43, mwaka 2022. Mashirika hayo yameishutumu Iran kwa kutumia hukumu ya kifo kueneza hofu katika jamii katikati mwa maandamano yaliyochochewa na kifo cha msichana Mahsa Amini Septemba mwaka 2022. Kwa mujibu wa mashirika ya kutetea haki za binadamu, adhabu ya kifo pia ilitekelezwa katika mashitaka mengine ikiwa ni pamoja na kesi zinazohusiana na madawa ya kulevya.

Ruka sehemu inayofuata Taarifa kuu ya DW

Taarifa kuu ya DW

Ruka sehemu inayofuata Taarifa zaidi kutoka DW