1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Iran: Marekani kuachia mali iliyofungiwa Qatar

11 Aprili 2026

Chanzo kimoja kikuu cha Iran kimesema leo kuwa Marekani imekubali ⁠kuachia mali ya Iran iliyofungiwa Qatar na benki nyingine za kigeni.

Pakistan Islamabad 2026 | Mazungumzo
Iran na Marekani kufanya mazungumzo ya kufikia makubaliano ya amani mjini Islamabad, Pakistan mnamo Aprili 11, 2026Picha: Wang Shen/Xinhua/dpa/picture alliance

Chanzo hicho kilichozungumza kwa sharti la kutotajwa jina kutokana na suala hilo kuwa nyeti, kimepongeza hatua hiyo na kuitaja kuwa ishara ya uzito wa kufikia makubaliano na Marekani katika mazungumzo mjini Islamabad nchini Pakistan.

Pia kimeliambia shirika la habari la Reuters kwamba kuachia mali hiyo kulihusishwa moja kwa moja na kuhakikisha usalama wa safari za meli katika  Mlango-Bahari wa Hormuz suala linalotarajiwa kuwa la kipaombele wakati wa mazungumzo hayo.

Hata hivyo, Marekani haijatoa tamko kuhusu suala hilo.

Tayari ujumbe wa Marekani unaoongozwa na naibu rais JD Vance umewasili Pakistan kwa mazungumzohayo na maafisa wa Iran ambao pia waliwasili mapema leo wakiongozwa na spika wa bunge Mohammad Bagher Qalibaf, yanayolenga kutafuta suluhisho la kudumu la vita Mashariki ya Kati.

 

Ruka sehemu inayofuata Taarifa kuu ya DW

Taarifa kuu ya DW

Ruka sehemu inayofuata Taarifa zaidi kutoka DW