Iran na Marekani zashambuliana kwa droni
28 Mei 2026
Hayo yalijiri saa chache baada ya Rais Donald Trumpkupinga ripoti kwamba anakaribia kufikia makubaliano na Tehran. Afisa huyo wa Marekani, ambaye aliomba kutotajwa jina lake ili kuzungumza waziwazi kuhusu operesheni za kijeshi, aliliambia shirika la habari la Reuters kwamba jeshi lilidungua ndege nne zisizo na rubani za Iran na kukipiga kituo cha operesheni katika mji wa bandari wa Bandar Abbas ambacho kilikuwa karibu kurusha droni ya tano.
Kikosi cha Walinzi wa Mapinduzi ya Kiislamu kimesema kiliilenga kambi ya Marekani kujibu kile kilichoelezea kama shambulio la mapema asubuhi la Marekani karibu na uwanja wa ndege wa Bandar Abbas. Kuwait - ambayo ina kambi kubwa ya Marekani - ilisema iliyajibu mashambulizi ya makombora na ndege zisizo na rubani bila kusema mashambulizi hayo yalitoka wapi.
Trump amesema mara kwa mara kwamba vita hivyo vinakarabia kumalizika lakini aliwaambia waandishi wa habari katika mkutano wa baraza la mawaziri Jumatano kwamba bado hajaridhika na mpango wa Iran na Marekani haijadili kuhusu kupunguza vikwazo dhidi yake.