Janga
Iran yaapa kushambulia mabenki ya Israel na Marekani
11 Machi 2026
Matangazo
Iran imesema mashambulizi yake yatalenga mabenki ya Israel na Iran baada ya benki yake kuu kushambuliwa na mahasimu wake hao.
Kamanda anayeongoza operesheni ya vita Khatam Al-Anbiya, amesema maadui wa taifa la Iran wameipa uhuru wa moja kwa moja nchi hiyo kushambulia maeneo hayo ya Israel na Marekani
Kulingana na mashirika ya habari ya Iran, shambulizi dhidi ya benki kuu ya Iran lililotokea usiku wa kuamkia leo limesababisha mauaji ya wafanyakazi wake kadhaa.
Hayo yanajiri wakati Kiongozi Mkuu mpya wa Iran Mojtaba Khamenei, akiwa bado hajasema lolote kuhusiana na vita vinavyoendelea siku tatu tangu alipochaguliwa kuchukua nafasi hiyo, baada ya baba yake Ayatollah Ali Khamenei kuuawa Februari 28.