1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Iran yaelezea hofu makabiliano ya Israel na Hezbollah

24 Septemba 2024

Wakati wa mkutano na waandishi habari mjini Tehran, msemaji wa serikali ya Iran Fatemeh Mohajerani, amesema nchi hiyo inalaani vikali mashambulizi hayo na kutaka uingiliaji wa haraka wa Baraza la Usalama la UN.

Watu wakiwa wamesimama karibu na gari lililoharibiwa, kwenye shambulizi la Israel  kusini mwa Beirut, Lebanon.
Watu wakiwa wamesimama karibu na gari lililoharibiwa, kwenye shambulizi la Israel kusini mwa Beirut, Lebanon.Picha: Amr Abdallah Dalsh/REUTERS

Iran leo imeelezea wasiwasi wake kuhusu  mashambulizi ya Israel dhidi ya Lebanon. Wakati wa mkutano na waandishi habari mjini Tehran, msemaji wa serikali ya Iran Fatemeh Mohajerani, amesema nchi hiyo inalaani vikali mashambulizi hayo na kutaka muingilio wa haraka wa Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa.

Tuna wasiwasi kuhusu hali ya kurudiwa kwa majanga kama yale yaliyotokea Gaza na Rafah, na kwa hivyo, tunataka uingiliaji wa haraka wa Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa."

Israel na kundi la Hezbollah linaloungwa mkono na Iran, leo zilikabiliana tena katika mashambulizi siku moja baada ya shambulizi kubwa la Israel kusababisha vifo vya takriban watu 500, maelfu kukimbia makazi yao kusini mwa Lebanon na kuziacha pande hizo mbili kwenye ukingo wa vita kamili.

 

Ruka sehemu inayofuata Taarifa kuu ya DW

Taarifa kuu ya DW

Ruka sehemu inayofuata Taarifa zaidi kutoka DW