1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Iran yakanusha ujenzi wa kituo cha siri cha nyuklia

16 Novemba 2025

Iran imekanusha juu ya kuwepo kwa kituo chochote cha siri cha urutubishwaji wa madini ya urani na kwamba miundombinu yake yote ipo chini ya uangalizi wa shirika la Umoja wa Mataifa linalosimamia nyuklia la IAEA.

Iran | Waziri wa Mambo ya Nje  Abbas Araghchi
Waziri wa Mambo ya Nje Iran Iranian Foreign Minister Abbas Araghchi Picha: Arif Hudaverdi Yaman/Anadolu/IMAGO

Hayo yamesema leo na Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran Abbas Araghchi na kuongeza kuwa hakuna urutubishaji wowote unaoendelea kwa sasa, baada ya vituo kuharibiwa katika uchokozi wa siku 12 wa Israel na Marekani ulipolekea vita baina yao ambavyo pia vilivuruga mazungumzo ya nyuklia kati ya Tehran na Washington.

Kauli hii ya Iran imetolewa baada ya vyombo vya habari nchini Marekani kuripoti kwamba Iran inaharakisha ujenzi wa kituo cha siri chini ardhi karibu na Natanz. 

Aidha Iran imetishia kukagua upya uhusiano wake na shirika la IAEA endapo azimio la kuipinga litapitishwa. Vita vya Juni viliharibu miundombinu na kusitisha mazungumzo ya nyuklia na Marekani, huku Iran ikisisitiza juu ya haki yake ya urutubishwaji wa madini ya urani "kwa matumizi chanya."