1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Iran yalaani hatua ya kurejeshewa vikwazo na UN

28 Septemba 2025

Iran imelaani vikali hatua ya kurejeshewa vikwazo na Umoja wa mataifa kuhusiana na mpango wake wa nyuklia, baada ya mazungumzo na mataifa ya magharibi kutofanikiwa pamoja na Israel na Marekani kushambulia vituo vyake.

Marekani, New York 2025 | Kikao cha Umoja wa Mataifa
Umoja wa MataifaPicha: Lev Radin/Pacific Press/picture alliance

Wizara ya Mambo ya Nje ya Iran imesema katika taarifa yake kwamba itatetea kwa uthabiti haki na maslahi yake ya kitaifa na kwamba hatua yoyote ya kukiuka haki na maslahi ya watu wake itakabiliana na majibu makali na kuongeza kwamba uamuzi huo hauna msingi wa kisheria ikiyataka mataifa kutoutambua uamuzi huo ilioutaja si halali.

Vikwazo hivyo vya vya Umoja wa mataifa vimeipiga marufuku Iran kuendeleza shughuli zinazohusiana na nyuklia na makombora ya masafa marefu, vimeanza kutumia kuanzia leo Jumapili. Hata hivyo mataifa ya Magharibi yamesisitiza kuwa bado meza ya mazungumzo iwa wazi.

Ruka sehemu inayofuata Taarifa kuu ya DW

Taarifa kuu ya DW

Ruka sehemu inayofuata Taarifa zaidi kutoka DW