SiasaIran
Iran yaondoa uwezekano wa kuzungumza na Marekani kwa sasa
1 Julai 2025
Matangazo
Araghchi alisema hayo kwenye mahojiano na kituo cha CBS Evening News cha Marekani, alipoulizwa kuhusu matamshi ya Rais Donald Trump kwamba mazungumzo ya nyuklia na Iran yanaweza kuanza tena mapema wiki hii.
Pamoja na hakikisho hilo, Araghchi amesema bado wanahitaji muda zaidi, ingawa milango ya diplomasia kamwe haitafungwa.
Marekani na Iran zilikuwa katika mazungumzo kuhusu mpango wa nyuklia wa Tehran wakati Israel iliposhambulia maeneo ya nyuklia ya Iran na miundombinu ya kijeshi, huku Marekani ikijiunga kwa kulipua maeneo matatu ya nyuklia ya Fordo, Natanz na Isfahan, mnamo Juni 21.