Migogoro
Iran yaonya hatari ya mabomu Mlango Bahari wa Hormuz
9 Aprili 2026
Matangazo
Jeshi la wanamaji la Iran limechapisha ramani inayoonesha eneo hatari katika Mlango Bahari wa Hormuz hasa sehemu zinakopita meli za biashara. Hayo yanajiri wakati Iran ikitishia kuwa itarejea kwenye mapigano kutokana na mashambulizi ya Israel dhidi ya Lebanon.
Utata wazidi uhusika wa Lebanon kwenye makubaliano ya kusitisha vita
Tehran inasisitiza kuwa kusimamisha mashambulizi Lebanon ni sehemu ya makubaliano ya kusitisha vita wakati Israel na Marekani zikipinga hilo.
Wakati huohuo wawakilishi wa Iran wanatarajiwa kuwasili mjini Islamabad baadaye leo kwa ajili ya mazungumzo ya usuluhishi na Marekani yanayosimamiwa na Pakistan.