MigogoroIran
Iran yathibitisha kifo cha afisa wa usalama Ali Larijani
18 Machi 2026
Matangazo
Shirika la habari la Fars, lenye mafungamano na Kikosi cha Walinzi wa Mapinduzi -IRGC- lilitangaza kuhusu kifo chake na kusema ameuawa kama "shahidi."
Larijani alihudumu kama mshauri wa karibu wa kiongozi mkuu Ayatollah Ali Khamenei, aliyeuawa katika shambulizi la anga Februari 28, siku ambayo vita vya Marekani na Israel dhidi ya Iran vilipozuka.
Tehran pia imethibitisha kifo cha kamanda wa vikosi vya usaidizi vya Basij, Brigedia Jenerali Gholam Reza Soleimani.
Shirika la habari la Fars lilichapisha taarifa ya kifo chake, ambapo Kikosi cha Walinzi wa Mapinduzi walimpongeza kwa "ushahidi wake wa heshima," huku kikisema wapiganaji wa Basij kamwe hawataacha kulipa kisasi cha kifo cha kiongozi wao.