1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Iran yaushambulia ubalozi wa Marekani mjini Riyadh

3 Machi 2026

Iran imeendelea usiku kucha kuvurumisha makombora ya masafa na droni kuilenga Israel na washirika wa Marekani kwenye eneo la ghuba, ikiwemo shambulizi kubwa lililoulenga ubalozi wa Marekani nchini Saudi Arabia.

Athari za mashambulizi ya Iran nchini Kuwait
Athari za mashambulizi ya Iran nchini Kuwait.Picha: AFP/Getty Images

Wizara ya Ulinzi ya Saudi Arabia imesema ndege mbili zisizo na rubani zimeushambulia ubalozi huo wa Marekani mjini Riyadh na kusababisha moto mkubwa ambao hata hivyo tayari umedhitiwa.

Rais Donald Trump ameapa kuiwajibisha Iran kwa uamuzi wake wa kuushambulia ubalozi wa nchi yake na kwa mauaji ya wanajeshi 6 wa Marekani tangu kuanza kwa vita Jumamosi iliyopita.

Mashambulizi ya kujibu mapigo ya Iran yamezifikia pia nchi za Bahrain na Kuwait huku makombora yake yaliyoelekezwa Israel yameanguka kwenye makaazi ya watu na kusababisha uharibifu.

Ruka sehemu inayofuata Taarifa kuu ya DW

Taarifa kuu ya DW

Ruka sehemu inayofuata Taarifa zaidi kutoka DW