1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Hamas iko tayari kutekeleza matakwa ya mpango wa Biden

16 Juni 2024

Kiongozi wa Hamas Ismail Haniyeh amesema majibu ya kundi hilo kwa pendekezo la kusitisha mapigano linaendana na kanuni zilizowekwa katika mpango uliotangazwa na rais wa Marekani Joe Biden.

Haniyeh
Kiongozi wa Hamas Ismail HaniyehPicha: Vahid Salemi/AP Photo/picture alliance

Akizungumza hii leo Haniyeh ameweka wazi kwamba kundi hilo na makundi mengine ya Wapalestina yako tayari kufanikisha pendekezo hilo linalojumuisha, kusitishwa kwa mapigano, kuondoka kwa wanajeshi wa Israel katika ukanda wa Gaza, kujengwa upya kwa mali iliyoharibiwa na makubaliano makubwa ya kubadilishana wafungwa pamoja na mateka wanaoendelea kuzuiliwa na kundi hilo la Hamas. 

Vita kati ya Israel na Hamas vimeingia mwezi wa saba

Tarehe 31 mwezi Mei, Biden alitangaza mpango wa awamu tatu ya pendekezo la Israel, lililojumuisha majadiliano ya kusitisha mapigano kikamilifu Gaza na kuachiwa kwa mateka wa Israel ili nao wafungwa wa Kipalestina waweze kuachiwa huru. 

Kando na kauli hiyo Israel na Hamas wameendelea kukataa vipengee muhimu katika mpango huo.

Ruka sehemu inayofuata Taarifa kuu ya DW

Taarifa kuu ya DW

Ruka sehemu inayofuata Taarifa zaidi kutoka DW