1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Israel bado inaendeleza mashambulizi yake Gaza

12 Septemba 2025

Wapalestina zaidi ya 40 wameuwawa kwenye mashambulizi ya Israel katika mji wa Gaza. Duru za hospitali zinasema wengi wa waliouwawa walitokea Gaza City

Gaza
Wapalestina zaidi ya 40 wameuwawa kwenye mashambulizi ya Israel mjini GazaPicha: Jack Guez/AFP/Getty Images

Mji huo ni makaazi ya wapalestina wengi waliojihifadhi huko licha ya amri ya serikali ya Israel ya kuwataka waondoke. Israel imetangaza nia yake ya kuudhibiti kikamilifu mji huo unaowahifadhi wapalestina takriban milioni moja.

Israel imesema itaendelea na mpango wake hadi pale wanamgambo wa Hamas watakapo sambaratishwa.

Walioshuhudia wanasema nyumba 15 ndani ya kambi kubwa ya wakimbizi, zililengwa kwa mashambulizi hayo ya angani.

Amjad Al-Shawa, kiongozi wa mtandao wa shirika lisilo la kiserikali la Palestina linalofanya kazi na Umoja wa Mataifa na makundi mengine ya kimataifa limesema asilimia 10 ya watu wa Gaza City wameuhama mji huo tangu Israel ilipotangaza mpango wake wa kuchukua udhibiti wa mji huo mwenzi mmoja uliopita.

 

Ruka sehemu inayofuata Taarifa kuu ya DW

Taarifa kuu ya DW

Ruka sehemu inayofuata Taarifa zaidi kutoka DW