1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Israel, Hezbollah zashambuliana baada ya mazungumzo Marekani

Josephat Charo
15 Aprili 2026

Israel na Hezbollah zimekabiliana tena kwa risasi Jumatano, siku moja baada ya mazungumzo ya kihistoria kati ya serikali za Israeli na Lebanon kuanza huko Washington, Marekani.

Uharibifu uliotokea katika eneo lililoshambuliwa na Israel kijiji cha kusini mwa Lebanon cha Abbasiyeh, nje ya mji wa Tiro Aprili 15, 2026.
Uharibifu uliotokea katika eneo lililoshambuliwa na Israel kijiji cha kusini mwa Lebanon cha Abbasiyeh, nje ya mji wa Tiro Aprili 15, 2026.Picha: Kawnat Haju/AFP

Israel na Hezbollah zimekabiliana tena kwa risasi leo Jumatano. Shirika la habari la Lebanon, NNA, limeripoti vifo kufuatia mashambulizi ya anga ya Israeli usiku kucha na mapema Jumatano kusini mwa Lebenon.

Jeshi la Israeli halijatoa kauli yoyote kuhusu ripoti hiyo, lakini limesema ni operesheni za ardhini zilizolengwa pekee ambazo zilikuwa zikiendelea kusini mwa Lebanon, zikilenga kulinda idadi ya watu kaskazini mwa Israel.

Wanamgambo wa Hezbollah wanaoungwa mkono na Iran walidai kuhusika na mashambulizi kadhaa kaskazini mwa Israeli, ambapo ving'ora vya kutoa onyo vilisikika. Jeshi la Israel limesema limerekodi takriban makombora 30 kutoka Lebanon mapema Jumatano.

Jumanne jioni, balozi wa Lebanon nchini Marekani, Nada Hamadeh Moawad, na mwakilishi wa Israel huko Washington, Jechiel Leiter, walifanya mazungumzo.

Kwa mujibu wa vyanzo vya Marekani, mazungumzo ya moja kwa moja yanatarajiwa kuendelea na yanaweza kusababisha makubaliano ya amani kamili.

Ruka sehemu inayofuata Taarifa kuu ya DW

Taarifa kuu ya DW

Ruka sehemu inayofuata Taarifa zaidi kutoka DW