1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Israel imeendelea kushambulia kambi ya wakimbizi ya Gaza

7 Juni 2024

Mashambulizi ya Israel yameitikisa kambi ya wakimbizi ya Gaza leo Ijumaa baada ya kushuhudiwa mashambulizi mengine yakifanyika dhidi ya shule moja inayosimamiwa na Umoja wa Mataifa.

Jengo lililoharibiwa vibaya baada ya mashambulizi ya Israel Gaza
Jengo lililoharibiwa vibaya baada ya mashambulizi ya Israel GazaPicha: Bashar Taleb/AFP/Getty Images

Katibu mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres ameyaelezea mashambulizi hayo kama mfano mwingine wa kutisha wa gharama wanayolipa raia katika vita hivyo.

Jana hospitali ya Al-Aqsa iliyoko katikati mwa Gaza ilisema takriban watu 37 waliuwawa katika shambulio lililofanywa dhidi ya kambi ya Nuseirat iliyoko kwenye shule ya Umoja wa mataifa.

Soma pia:Israel yaishambulia Gaza baada ya mpango wa amani kukwama

Juhudi za kidiplomasia za kusimamia upatikanaji wa makubaliano ya kusitisha vita zinaonesha zimekwama, wiki moja baada ya rais wa Marekani Joe Biden kupendekeza mpango mpya wa hatua tatu wa usitishaji vita hivyo.

Bado kundi la wanamgambo la Hamas halijatowa jibu lake juu ya mpango huo uliopendekezwa,wakati Israel imeonesha msimamo wake waziwazi ikisisitiza kuendelea na vita hivyo kwa lengo la kutaka kuliangamiza kabisa kundi hilo la wanamgambo la Palestina.

Ruka sehemu inayofuata Taarifa kuu ya DW

Taarifa kuu ya DW

Ruka sehemu inayofuata Taarifa zaidi kutoka DW