1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW
SiasaIsrael

Israel: Bado hakuna makubaliano ya kuachiliwa mateka

19 Novemba 2023

Waziri Mkuu wa Israel Benjamin Netanyahu pamoja na maafisa wa Marekani wamesisitiza kwamba bado hakujafikiwa makubaliano ya kuwezesha mateka wao kuachiliwa.

Waziri Mkuu wa Israel Benjamin Netanyahu akionyesha ramani yake mpya ya "Mashariki ya Kati Mpya"
Septemba 22, 2023, Waziri Mkuu wa Israel Benjamin Netanyahu akiwa ameshika ramani ya "Mashariki ya Kati Mpya" wakati akihutubia Mkutano wa Hadhara Kuu ya 78 ya Umoja wa Mataifa. Picha: Richard Drew/AP Photo/picture alliance

Mateka hao wanashikiliwa na wanamgambo wa Hamas na makubaliano yangewezesha kuachiliwa kwa idadi kubwa ya mateka wanawake na watoto.

Hii ni baada ya gazeti la Washington Post la Marekani kuripoti kwamba Israel na Hamas wamekubaliana kusitisha mapigano kwa muda wa siku hizo tano ili kuruhusu mchakato huo.

Netanyahu amewaambia waandishi wa habari katika mkutano jana jioni ambapo alisisitiza kwamba hakuna makubaliano yaliyofikiwa hadi sasa na ameahidi kutoa taarifa patakapokuwa na jambo lolote.

Msemaji wa masuala ya usalama wa taifa wa Ikulu ya Marekani, Adrienne Watson pia amezipuuza ripoti hizo na kuandika kupitia ukurasa wake wa X kwamba makubaliano hayo hayajafikiwa, ingawa wanaendelea na jitihada. 

Hamas, waliposhambulia kusini mwa Israel, mnamo Oktoba 7 walichukua mateka watu 240 na watu wengine 1,200 waliuawa.

Ruka sehemu inayofuata Taarifa kuu ya DW

Taarifa kuu ya DW

Ruka sehemu inayofuata Taarifa zaidi kutoka DW