MigogoroMashariki ya Kati
Israel na Lebanon zakubaliana kuandaa mazungumzo mengine
15 Aprili 2026
Matangazo
Tangazo hilo limetolewa baada ya kukamilika kwa mashauriano hayo yaliyodumu kwa zaidi ya saa mbili kati ya wawakilishi wa Israel na Lebanon chini ya upatanishi wa Waziri wa Mambo ya Kigeni wa Marekani, Marco Rubio.
Ofisi ya Rubio imesema pande zote mbili zimekubaliana kufanya mazunungumzo ya moja kwa moja katika eneo na muda utakaoafikiwa kwa pamoja.
Hayo yalikuwa mashauriano ya kwanza kati ya nchi hizo mbili jirani ambazo zimetumbukia kwenye uhasama wa muda mrefu kutokana na harakati za kundi laHezbollah la nchini Lebanon lenye mafungamano ya karibu na Iran. Israel imesema inataka kushirikiana na serikali ya Lebanon kulipokonya silaha kundi hilo.