Israel: Utambuzi wa taifa la Palestina ni 'tuzo kwa ugaidi'
10 Aprili 2025
Matangazo
Katika taarifa yake kwenye mtandao wa kijamii wa X jana jioni, Saar alisema kutambuliwa kwa upande mmoja kwa taifa la Palestina na nchi yoyote ile, hakutaleta amani, usalama na utulivu katika kanda hiyo, lakini kinyume chake itawasukuma mbali zaidi.
Macron asema Ufaransa inapanga kulitambua taifa la Palestina
Jumatano, Rais Macron alisema kuwa Ufaransa inapanga kulitambua taifa la Palestina ndani ya miezi kadhaa na huenda ikachukuwa hatua hiyo wakati wa mkutano wa Umoja wa Mataifa mjini New York mwezi Juni.
Rais huyo ameongeza kuwa lengo lao ni kuongoza mkutano huo na Saudi Arabia mwezi Juni, ambapo wanaweza kukamilisha mchakato huo wa kutambuliwa na mataifa kadhaa.