Israel yaendelea kuishambulia Iran
3 Machi 2026
Matangazo
Vishindo vya makombora vilisika mnamo usiku wa kuamkia leo mjini Tehran na kituo cha telesheni nchini Iran cha Press TV kiliripoti makao makuu ya IRIB yalishambuliwa.
Mashambulizi hayo ni mwendelezo wa hujuma nzito za kijeshi zilizofanywa kutwa nzima jana Jumatatu na vikosi vya Israel nchini Iran. Rais Donald Trump wa Marekani aliwaambia waandishi habari mjini Washington kwamba vita hivyo vinaweza kuendelea kwa muda wa wiki tano na zaidi.
Utawala wake umeionya Iran kujiandaa kwa mashambulizi makubwa zaidi yatakayoisambaratisha miundombinu ya kijeshi ya nchi hiyo.