1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Israel yapokea miili mitatu ya mateka kutoka kwa Hamas

3 Novemba 2025

Israel imesema imepokea miili ya mateka watatu kutoka kwa wanamgambo wa Hamas.

Israel Rishon LeZion 2025 | Begräbnis der getöteten Geisel Yossi Sharabi
Picha: Leo Correa/AP Photo/picture alliance

Hii ni kama sehemu ya mpango wa kubadilishana wafungwana mateka ulioko chini ya makubaliano ya kusitisha vita yaliyosimamiwa na Marekani.

Msemaji wa wizara ya afya ya Israel amesema kuwa miilihiyo imewasili katika kituo cha kitaifa cha uchunguzi kwa ajili ya utambuzi na uchunguzi wa mazingira na sababu za vifo.

Wanamgambo wa Hamas wamesema wameipata miili hiyo katika njia mojawapo ya kuelekea kwenye mahandaki ya kusini mwa Ukanda wa Gaza.

Wanamgambo hao walikuwa wakiwashikilia mateka 48 huko Gaza wakiwemo 20 ambao walithibitishwa kuwa hai wakati makubaliano ya kusitisha mapigano yalipotangazwa.

Tangu kuanza utekelezwaji wa makubaliano hayo, Hamas imewaachia mateka wote waliokuwa hai na ikaanza mchakato wa kuiwasilisha miili ya mateka 28 waliofariki dunia.

Israel inaituhumu Hamas kwa kujikokota katika zoezi hilo la kuirejesha miili hiyo ila wanamgambo hao wanalalamikia ugumu wa kuifukua miili hiyo iliyofunikwa na vifusi vya majengo.

Ruka sehemu inayofuata Taarifa kuu ya DW

Taarifa kuu ya DW

Ruka sehemu inayofuata Taarifa zaidi kutoka DW