Israel yasema imemuuwa mkuu wa usalama wa Iran Ali Larijani
17 Machi 2026
Ripoti zilizochapishwa muda mfupi uliopita na shirika la habari la AP zimesema, mkuu wa usalama wa taifa wa Iran Ali Larijani ameuwawa. Shirika hilo limemnukuu waziri wa ulinzi wa Israel, Israel Katz.Vita na ukandamizaji vyazidisha kiwewe kwa Wairan
Iran haijathibitisha ripoti hizo. Vyombo vya habari vya Israel awali viliripoti juu ya kulengwa kwa mkuu huyo wa usalama wa Iran lakini havikwenda umbali wa kuthibitisha mara moja juu ya kuuliwa kwake.Jeshi la Israel limetangaza kuanzisha mashambulio mapya ikiyalenga maeneo mbali mbali ya miji ya Tehran na Beirut.
Kwa upande mwingine mashambulizi ya droni na makombora ya Iran dhidi ya Umoja wa Falme za Kiarabu yamesababisha mripuko kwenye tenki ya mafuta katika eneo la pwani la mashariki mwa nchi hiyo linalopakana na Oman.Vita vya Marekani-Israel na Iran
Taarifa za kushambuliwa kwa mara nyingine eneo la Fujairah, zimekuja baada ya UAE kufunga kwa muda anga yake kufuatia vitisho mashambulio ya Iran.
Vita hivyo vya Mashariki ya kati na Ghuba mpaka sasa vimesababisha mauaji ya watu 1,300 nchini Iran, takriban 850 Lebanon na watu 12 Israel kwa mujibu wa maafisa wa nchi hizo.
Jeshi la Marekani limesema wanajeshi wake 13 wameuwawa na wengine kiasi 200 wamejeruhiwa.