1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Israel yasema mashambulizi dhidi ya Iran kuongezeka

21 Machi 2026

Waziri wa Ulinzi wa Israel Israel Katz, amesema leo kuwa mashambulizi ya Israel na marekani dhidi ya Iran "yataongezeka mno" wiki ijayo.

Lebanon Nabatieh 2025 | shambulizi la Israel
Shambulizi la israel kusini mwa Lebanon mnamo Novemba 22, 2025Picha: Ramiz Dallah/Anadolu Agency/IMAGO

Katz amesema hayo katika taarifa kwa njia ya video, saa chache baada ya Rais wa Marekani Donald Trump kusema kuwa anafikiria kumaliza operesheni za kijeshi Mashariki ya Kati, licha ya nchi hiyo kutangaza kutuma meli zaidi za kivita na jeshi la wanamaji katika eneo hilo huku Iran ikitishia kushambulia maeneo ya utalii duniani kote.

Mapema leo, jeshi la Israel limesema limekuwa likilenga shabaha zake ndani ya Tehran.

Tangazo hilo limekuja muda mfupi baada ya jeshi hilo kusema limeanza wimbi la mashambulizi kulenga maeneo ya Hezbollah katika vitongoji vya kusini mwa Beirut nchini Lebanon.

 

Ruka sehemu inayofuata Taarifa kuu ya DW

Taarifa kuu ya DW

Ruka sehemu inayofuata Taarifa zaidi kutoka DW