1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Israel yasema wakati umefika kufikiria juu ya Ukanda wa Gaza.

Abdu Said Mtullya16 Juni 2010

Israel yafikiria kulegeza sukurubu Ukanda wa Gaza?

Waziri Mkuu wa Israel Benjamin Netanyahu.Picha: AP

Kutokana na ongezeko la shinikizo la kimataifa Israel sasa inafikiria kulegeza masharti ya kuifunga mipaka ya Ukanda wa Gaza.

Msemaji wa serikali ya Israel amefahamisha kwamba waziri Mkuu Benjamin Netanyahu ,leo atakutana na baraza lake la mawaziri , kujadili juu ya kuirefusha orodha ya mahitaji yanayoweza kuruhusiwa kuingizwa katika Ukanda wa Gaza- sehemu inayodhibitwa na Hamas.

Waziri wa masuala ya kijamii Isaac Herzog amesema wakati sasa umefika wa kubadili namna ambayvo mipaka ya Ukanda wa Gaza imekuwa inafungwa.

Lakini Israel wakati wote imekuwa inahoji kwamba imeifunga mipaka ya Ukanda wa Gaza ili kuzuia silaha kupenyezwa kwa ajili ya Hamas.

Ruka sehemu inayofuata Taarifa kuu ya DW

Taarifa kuu ya DW

Ruka sehemu inayofuata Taarifa zaidi kutoka DW