Israel yasema wanautambua uhuru wa Ukraine
16 Februari 2023Matangazo
Bila ya kuitaja Urusi, Cohen amesema Israel inasimama pamoja na Ukraine na itaendelea kushikamana na watu wa Ukraine pamoja na kuutambua uhuru na uadilifu wa taifa hilo.
Amesema hayo kwenye mkutano na waandishi wa habari pamoja na mwenzake wa Ukraine, Dymitro Kuleba.
Soma pia:Vita vya Urusi, Ukraine vyatawala sherehe za Carnival
Aidha, amesema, Israel inaweza kusaidia jitihada za Umoja wa Mataifa za kupatikana kwa amani wiki ijayo na kusaidia upatikanaji wa dola milioni 200 zitakazopelekwa kwenye miradi ya afya na miundombinu.