MigogoroMashariki ya Kati
Israel yashambulia Lebanon kujibu maroketi ya Hezbollah
2 Machi 2026
Matangazo
Mashuhuda wamesema zaidi ya mitikisiko 12 ya makombora imesikika mjini Beirut katika mashambulizi yaliyo makali zaidi kufanywa na Israel nchini Lebanon tangu vita vyake na Hezbollah vya mwaka 2024.
Kundi la Hezbollah lenye ushawishi mkubwa wa kisiasa ndani ya Lebanon limesema limeilenga Israel kwa maroketi na droni ili kuonesha mshikamano na Iran na kulipa kisasi kwa kuuliwa Khamenei.
Ingawa hivi sasa nguvu za kundi hilo zimepungua tangu vita vya mwaka 2024, Israel inasema bado linao uwezo fulani wa kijeshi wa kupanga na kushambulia.