1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Israel yatambua mwili wa mateka uliorejeshwa kutoka Gaza

8 Novemba 2025

Israel imetambua mabaki ya mateka wa hivi karibuni zaidi kurejeshwa na kundi la Hamas kutoka Gaza na kubakisha idadi ya miili mitano mingine inayopaswa kurejeshwa chini ya makubaliano ya amani yaliyosimamiwa na Marekani.

Palestina, Khan Yunis 2025 | Miili ya Wapalestina
Miili ya Wapalestina iliyokuwa inashikiliwa na IsraelPicha: Abed Rahim Khatib/Anadolu/picture alliance

Jeshi la Israel limeutambua mwili huo uliorejeshwa jana kuwa wa dereva aliyejitolea wa gari ya wagonjwa, Lior Rudaeff, ambaye aliuawa katika shambulizi la Hamas la Oktoba 7, 2023 lililoanzisha vita vya Gaza.

Rudaeff, Muisraeli mwenye asili ya Argentina alikuwa na umri wa miaka 61 wakati wa shambulio hilo na ni mmoja wa raia watano waliokuwa na silaha aliyeuawa alipokuwa akijaribu kutetea jamii yake ya Nir Yitzhak Kibbutz.

Kundi la Familia za Mateka na Waliopotea la Israel, limepongeza hatua ya kurejeshwa kwa mwili huo na kusema inaleta faraja kwa familia za waathiriwa.

 

Ruka sehemu inayofuata Taarifa kuu ya DW

Taarifa kuu ya DW

Ruka sehemu inayofuata Taarifa zaidi kutoka DW