1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Israel kukifungua kivuko muhimu cha Rafah

15 Oktoba 2025

Israel inatarajiwa Jumatano kuruhusu kufunguliwa kwa kivuko cha Rafah ili kuwezesha misaada zaidi ya kibinaadamu kuingizwa katika Ukanda wa Gaza.

Rafah | Malori ya misaada yakijiandaa kupita kwenye kivuko cha Rafah kwenda Gaza
Malori ya misaada yakijiandaa kupita kwenye kivuko cha Rafah kuelekea GazaPicha: STR/AFP/Getty Images

Hatua hii ni sehemu ya makubaliano ya kusitisha mapigano yaliyosimamiwa na Marekani. Takriban malori 600 yaliyosheheni msaada wa chakula, dawa pamoja na vifaa vinavyohitajika kukarabati miundombinu iliyoharibiwa na vita, yanatarajiwa kuruhusiwa kuingia Gaza.

Siku ya Jumanne, Israel ilitishia kukifunga  kivuko hicho muhimu cha Rafah kinachopakana na nchi ya Misri baada ya kudai kuwa Hamas ilishindwa kuheshimu makubaliano hayo kwa kutokabidhi miili ya mateka waliosalia. Lakini baadaye Hamas waliikabidhi miili ya mateka hao wanne. Mashirika ya misaada yametoa wito wa kuongeza mtiririko wa misaada huko Gaza wakisema kuwa mahitaji ni makubwa mno.

 

Ruka sehemu inayofuata Taarifa kuu ya DW

Taarifa kuu ya DW

Ruka sehemu inayofuata Taarifa zaidi kutoka DW