1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Israel yatishia kuushambulia zaidi Ukanda wa Gaza

3 Novemba 2025

Israel imetishia kuanzisha tena mashambulizi ya kijeshi katika Ukanda wa Gaza na kuzuwia misaada kuingia katika ukanda huo, iwapo kundi la wanamgambo wa Hamas litajikokota kuiachilia miili ya mateka iliosalia Gaza.

Israel Jerusalem 2025 | Waziri Mkuu wa Israel Benjamin Netanyahu
Israel yatishia mashambulizi Gaza ikiwa mabaki ya miili ya mateka wake Picha: Alex Kolomoisky/REUTERS

Mpaka sasa kundi hilo tayari limewaachia mateka 20 walio hai wa Israel baada ya makubaliano ya usitishaji mapigano baina yao na Israel.

Lakini mchakato wa kuirudisha miili nane iliyosalia umekuwa wa polepole mno. Kundi hilo limekuwa likiachia mwili mmoja mmoja au miwili kila baada ya siku chache.

Maadai ya Hamas ni kwamba haijaweza kuyafikia mabaki yote ya miili kwa sababu yako chini ya vifusi vilivyotokana na mashambulizi ya Israel katika Ukanda huo wa Gaza.

Israel yenyewe tayari imerudisha miili ya Wapalestina 225  iliyokuwa inaizuiliwa nchini mwake bila kutoa maelezo yeyote kuhusu utambulisho wao.

 

Ruka sehemu inayofuata Taarifa kuu ya DW

Taarifa kuu ya DW

Ruka sehemu inayofuata Taarifa zaidi kutoka DW