1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW
SiasaIsrael

Israel yawapiga risasi wanaodaiwa wapiganaji 3 wa Palestina

25 Julai 2023

Jeshi la Israel limesema limewapiga risasi na kuwaua watu 3 wanaodaiwa kuwa wapiganaji wa Palestina leo katika eneo la kaskazini la Ukingo wa Magharibi unaokaliwa kwa mabavu.

Israel, Westbank, Nablus | Konflikt in den Palästinensischen Gebieten
Picha: picture-alliance

Vikosi vya usalama vya Israel vimesema vilijibu mashambulizi ya risasi kutoka kwa wapiganaji wa Kipalestina waliowakuwamo kwenye gari moja katika mji wa Nablus, ambao ndio mji mkuu wa kibiashara wa eneo hilo na kiini cha mashambulizi ya hivi karibuni ya jeshi la Israeli.

Soma pia:Makundi ya itikadi kali yasema vikosi vya usalama vya Palestina vimewakamata wafuasi wake watano mjini Jenin

Vyombo vya habari vya Palestina vimeelezea mauaji hayo ya Israel kuwa tukio la kuvizia kufuatia jaribio la wanamgambo hao wa Palestina kushambulia vikosi vya Israel karibu na makaazi ya Wayahudi yaliyoko karibu na Nablus. Jeshi la Israel limesema limekamata bunduki tatu aina ya M-16 na silaha nyengine kwenye gari hilo.

Ruka sehemu inayofuata Taarifa kuu ya DW

Taarifa kuu ya DW

Ruka sehemu inayofuata Taarifa zaidi kutoka DW