Taifa la Israel linaadhimisha miaka 70 tangu lilipoundwa. Katika sherehe hizo zinazoendelea, Waziri mkuu wa nchi hiyo Benjamin Netanyahu amesema Israel imekuwa taifa kubwa ambalo litashinda ''giza'' la maadui zake. Wakati huo huo Wapalestina wanakumbuka siku waliyopoteza ardhi zao, na kuingia ukimbizini au katika ardhi zinazokaliwa na Israel kimabavu.