1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

JAKARTA: Juhudi za uokoaji zaendelea kuwatafuta waathiriwa wa mkasa wa feri.

1 Januari 2007

Kikosi cha wanamaji cha Indonesia kimeongeza juhudi zake kuwatafuta watu walioathirwa na mkasa wa feri uliotokea siku ya Ijumaa katika pwani ya Java.

Manusura walikaa baharini kwa usiku wa tatu kutokana na juhudi za uokoaji kutatizwa na hali mbaya ya hewa.

Mamia ya watu wamearifiwa kutoweka baada ya wavuvi na makundi ya uokoaji kufanikiwa kupata watu mia mbili miongoni mwa watu zaidi ya mia sita waliokuwa katika feri hiyo.

Maiti zaidi ya sitini zimeopolewa.

Feri hiyo iliyozama siku ya Ijumaa usiku, ilikuwa safarini kutoka kisiwa cha Borneo ikielekea bandari ya Semarang, Java
Ruka sehemu inayofuata Taarifa kuu ya DW

Taarifa kuu ya DW

Ruka sehemu inayofuata Taarifa zaidi kutoka DW