Jamaa wa waandishi wanaozuiliwa hawataonana Iran
27 Desemba 2010Matangazo
Kwa mujibu wa msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje ya Ujerumani,jamaa hao hawataweza kukutana katika kipindi hiki cha Krismasi kama walivyoahidiwa na serikali ya Iran.Awali,akihojiwa na Gazeti la Bild Am Sonntag,Waziri wa Mambo ya Nje wa Ujerumani,Guido Westerwelle,alisema kuwa huenda wakakutana wakati huu.Waandishi hao wawili wa habari wa gazeti la Bild Am Sonntag walikamatwa mwezi wa Oktoba walipouwa wakiwahoji mtotto wa kiume na wakili wa Sakineh Mohammadi Ashtiani aliyehukumiwa kifo kwa kupigwa mawe.Mwanamke huyo aliye na umri wa miaka 43 alikatiwa hukumu hiyo kwasababu ya mashtaka ya zinaa.Waandishi hao wa habari waliingia Iran kw akutumia vibali vya watalii.