1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW
SiasaJamhuri ya Kongo

Jamhuri ya Kongo yajiandaa kwa uchaguzi wa Rais

13 Machi 2026

Wapiga kura nchini Kongo-Brazzaville wanaelekea vituoni Jumapili ya wiki hii kwa uchaguzi mkuu ambao inaaminika utampatia muhula mwingine rais wa muda mrefu Dennis Sassou N'Guesso.

Rais Dennis Sassou N'Guesso wa Jamhuri ya Kongo
Rais Dennis Sassou N'Guesso wa Jamhuri ya Kongo.Picha: Getty Images

Kiongozi huyo mwenye umri wa miaka 82, na ambaye aliingia madarakani mwaka 1979, atachuana na wanasiasa wengine sita wasio na ushawishi baada ya vyama vikuu vya upinzani kuamua kutosimamisha wagombea.

Vigogo wawili wa upinzani Jean-Marie Michel Mokoko na André Okombi Salissa ambao inaaminika wangetoa changamoto kwa Rais N´Guesso wako gerezani kwa karibu muongo mmoja baada ya kukutwa na hatia ya kuhatarisha usalama wa taifa.

Licha ya utajiri mkubwa wa mafuta, Jamhuri ya Kongo inakabiliwa na mzigo wa madeni na uchumi unaodorora, huku viwango vya ukosefu wa ajira kwa vijana vimefikia asilimia 24.

Ruka sehemu inayofuata Taarifa kuu ya DW

Taarifa kuu ya DW

Ruka sehemu inayofuata Taarifa zaidi kutoka DW