Uamuzi wa Mahakama ya Katiba Afrika Kusini kuruhusu wanaume kuchukua majina ya wake zao umeibua mjadala mkubwa. Wanaharakati wa usawa wa kijinsia wameupongeza uamuzi huo kama hatua ya kuvunja mfumo dume na kuleta usawa katika ndoa. Hata hivyo, wafuasi wa mila za jadi wanasema wanaume kuchukua majina ya ukoo ya wake zao ni tishio kwa utambulisho wa ukoo wa kiume, wakihofia kupotea kwa nasaba zao.