Jepchirchir kutoka Kenya ashinda mbio za marathon Japan
14 Septemba 2025
Matangazo
Wanariadha hao wawili walimaliza mbio hizo kwa kuingia katika uwanja wa kitaifa wa Japan bega kwa bega baada ya kukimbia kilomita 42 katika barabara za Tokyo
Assefa alionekana kusonga mbele kabla ya Jepchirchir aliyeshinda medali ya dhahabu katika michezo ya olimpiki mwaka 2021 nchini Japan kuonesha nguvu zake katika dakika za mwisho na kushinda kwa kukimbia kwa saa 2 dakika 24 na sekundu 43
Assifa alichukua nafasi ya pili akiwa nyuma kwa sekunde mbili pekee.
Mwanariadha wa Uruguay Julia Paternain aliweka historia kwa kuchukua medali ya shaba na kuwa mwanariadha wa kwanza kuchukua ushindi wa medali nchini humo.