1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

JERUSALEM Fischer azuru Israel

14 Julai 2005

Waziri wa mambo ya kigeni wa Ujerumani bwana Joschka Fischer, amelilaani shambulio la bomu la kujitoa muhanga lililofanywa katika mji wa Netanya nchini Israel. Wakati wa mkutano wake pamoja na waziri wa mambo ya kigeni wa Israel, Silvan Shalom, Fischer amesema magaidi ni lazima watengwe mbali na jamii.

Waziri mkuu wa Israel Ariel Sharon amemshukuru Fischer kwa hatua ya Ujerumani kujitolea kikamilifu katika mpango wa kutafuta amani ya mashariki ya kati.

Waziri Fischer ameahidi kwamba Ujerumani na umoja wa Ulaya zinaiunga mkono Israel katika mpango wake wa kuyaondoa makazi ya walowezi wa kiyahudi kutoka mkanda wa Gaza. Umoja wa Ulaya unataka kusaidia katika ujenzi wa taasisi nchini Palestina ili kudumisha utulivu huko Gaza.

Ruka sehemu inayofuata Taarifa kuu ya DW

Taarifa kuu ya DW

Ruka sehemu inayofuata Taarifa zaidi kutoka DW