JERUSALEM: Israel imekataa kusitisha mapigano
30 Julai 2006Matangazo
Israel imekataa ombi la mratibu wa misaada ya dharura wa Umoja wa Mataifa,Jan Egeland,alietaka mapigano yasitishwe kwa muda wa siku tatu ili misaada iweze kupelekwa kusini mwa Lebanon.Kwa mujibu wa msemaji wa serikali ya Israel,tayari kuna barabara zinazoruhusu misafara ya kupeleka misaada ya kiutu.Akasema,ikiwa mapigano yatasitishwa,nafasi hiyo huenda ikatumiwa na Hezbollah kujipatia upya silaha na mahitaji mengine.Wakati huo huo misaada imewasili Beirut kwa njia ya ndege na meli kutoka Misri, Jordan,Umoja wa Falme za Kiarabu na Marekani.
