JERUSALEM ;Solana ailaumu Israel
12 Julai 2005Matangazo
Mshauri wa masuala ya nchi za nje wa Umoja wa Ulaya bwana Javier Solana ameilamu Israel kwa kujenga ukuta utakaowatenga wapalestina.
Bwana Solana amesema ,kisheria ukuta huo haustahili kujengwa panapokusudiwa kwa kuwa utasababisha matatizo makubwa kwa wapalestina.
Hatahivyo bwana Solana amesema mjini Jerusalem , kwamba Israel ina haki ya kujilinda na ameunga mkono mpango wa nchi hiyo juu ya kuondoka ukanda wa Gaza.
.