1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

JERUSALEM: Steinmeier ziarani Mashariki ya Kati

9 Agosti 2006

Waziri wa mambo ya kigeni wa Ujerumani,Frank-Walter Steinmeier amekutana na waziri wa ulinzi wa Israel,Amir Peretz mjini Jerusalem.Steinmeier anakutana pia na waziri mkuu wa Israel Ehud Olmert na waziri mwenzake wa kigeni Zippi Livni, kujadili njia ya kuumaliza mgogoro wa Lebanon. Siku ya Jumanne alipokutana na waziri mkuu wa Lebanon Fuad Siniora,waziri Steinmeier alisema pendekezo la Beirut kuwa ipeleke kikosi chake cha wanajeshi 15,000 kusini mwa Lebanon,huenda likaiimarisha serikali ya Lebanon.

Ruka sehemu inayofuata Taarifa kuu ya DW

Taarifa kuu ya DW

Ruka sehemu inayofuata Taarifa zaidi kutoka DW