1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

JERUSALEM : Steinmeir azuru Israel

10 Agosti 2006

Waziri wa mambo ya nje wa Ujerumani Frank Walter Steinmeir amesema anaona kuna fursa ya kufikiwa kwa suluhisho la kidiplomasia katika mzozo kati ya Israel na Hezbollah.

Baada ya mazungumzo mjini Jerusalem na Waziri Mkuu Ehud Olmert hapo jana Steinmeir amesema usitishaji wa mapigano unaweza kufikiwa chini ya msingi wa azimio la Umoja wa Mataifa ambalo hivi sasa linashughulikiwa na Baraza la Usalama.

Steinmeir pia ameelezea wasi wasi mkubwa juu ya hali ya maafa ya kibinaadamu nchini Lebanon.

Awali Steinmeir alikuwako mjini Beirut ambapo alikutana na viongozi wa Lebanon.

Ruka sehemu inayofuata Taarifa kuu ya DW

Taarifa kuu ya DW

Ruka sehemu inayofuata Taarifa zaidi kutoka DW