Jeshi la Iran lasema limelenga kambi za kijeshi za Israel
12 Machi 2026
Matangazo
Katika taarifa kupitia televisheni ya kitaifa, jeshi la Iran limesema kuwa kambi za jeshi la anga za Palmachim na Ovda za utawala wa Kizayuni pamoja na makao makuu ya Shin Bet zililengwa kwa droni.
Wakati huo huo, mashambulizi ya Marekani na Israel dhidi ya Iran, yameharibu takriban maeneo manne ya kitamaduni na kihistoria, yakiwemo makasri na msikiti wa kale, hali inayoibua wasiwasi kuhusu athari za vita hivyo vinavyopanuka dhidi ya maeneo yanayolindwa ambayo ni muhimu kwa utambulisho wa Iran na historia ya dunia.
Uharibifu huo umezisukuma Iran na Lebanon kutuma ombi wiki hii kwa Shirika la Umoja wa Mataifa la Elimu Sayansi na Utamaduni, UNESCO, kuongeza maeneo zaidi kwenye orodha yake ya ulinzi iliyoimarishwa.