1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW
SiasaAsia

Jeshi la Pakistan lawaua wanamgambo 30

20 Novemba 2025

Vikosi vya Pakistan vimewaua wanamgambo 30 katika operesheni kadhaa karibu na eneo la mapambano na Afghanistan katika siku za hivi karibuni.

Wana, Pakistan 2025 |Shambulizi katika chuo cha kijeshi
Wanajeshi wa Pakistan wakiwa kwenye mji wa Wana unaopakana na AfghanistanPicha: Ahsan Shahzad/AP Photo/picture alliance

Jeshi la Pakistan limesema hayo Alhamisi baada ya mshambuliaji wa kujitoa muhanga kuwaua watu 12 wiki iliyopita mjini Islamabad.

Wanamgambo 23 waliuawa katika mashambulizi ya wilaya ya Kurram kwenye jimbo la Khyber Pakhtunkhwa jana.

Katika taarifa iliyofuata, jeshi limesema wanamgambo wengine saba waliuawa katika operesheni tatu tofauti kwenye wilaya za Mohmand, Lakki Marwat na Tank Novemba 18 na 19.

Mapambano dhidi ya wanamgambo kuendelea

Jeshi limesema Pakistan itaendelea kupambana na kuondoa kitisho cha ugaidi unaofadhiliwa na kuungwa mkono na mataifa ya kigeni.

Mara kwa Mara Pakistan imekuwa ikiishutumu nchi jirani ya Afghanistan kwa kuyahifadhi makundi ya wanamgambo, na hasa kundi la Tehreek-e-Taliban, TTP, ambalo hufanya mashambulizi nchini Pakistan.

 

Ruka sehemu inayofuata Taarifa kuu ya DW

Taarifa kuu ya DW

Ruka sehemu inayofuata Taarifa zaidi kutoka DW