SiasaSomalia
Jeshi la Somalia latwaa udhibiti Jimbo la Kusini Magharibi
31 Machi 2026
Matangazo
Wanajeshi wa Somalia waliripotiwa kuingia kwenye mji mkuu wa jimbo hilo, Baidoa, siku ya Jumatatu (Machi 30).
Baidoa ni wa kimkakati wenye makao makuu ya kikosi cha kimataifa wa walinda amani na mashirika kadhaa ya kibinaadamu, kwenye eneo hilo lililoathirika kwa ukame, migogoro na wakimbizi wa ndani.
Rais wa jimbo hilo, Abdiaziz Hassan Mohamed Laftagareen, aliandika kupitia mtandao wa Facebook kuwa amejiuzulu wadhifa wake, siku chache baada ya kuchaguliwa kuongoza tena kwa muhula mwengine wa miaka mitano.
Wakaazi wengi wameukimbia mji wa Baidoa na baadhi ya mashirika ya misaada yamesitisha shughuli zao, wakihofia mapigano kati ya wanajeshi wa serikali kuu na vikosi vya jimbo hilo.