MigogoroSudan
Jeshi la Sudan lasema limezuia shambulizi la RSF
26 Novemba 2025
Matangazo
Jeshi hilo lilizuia shambulizi kwenye kambi yake katika mji wa kimkakati wa Babanusa ambao ni ngome yake kubwa ya mwisho katika eneo hilo.
Babanusa iko kwenye njia muhimu ya usafirishaji kati ya mji mkuu Khartoum kupitia Kordofan na Darfur.
Mapema jana, mjumbe wa Marekani barani Afrika, Massad Boulos alisema akiwa Abu Dhabi kwamba pande zote hazijakubaliana na pendekezo jipya la kusitisha mapigano lililoandaliwa na kundi la Quad linalojumuisha Marekani, Saudi Arabia, Umoja wa Falme za Kiarabu na Misri.