1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Bayern yashinda taji la 13 la Bundesliga katika miaka 14

Josephat Charo
20 Aprili 2026

Bayern Munich ilishinda taji jingine la Bundesliga Jumapili, la 13 kwa klabu hiyo katika miaka 14, baada ya msimu uliovunja rekodi ambao bado unaweza kuwa bora zaidi.

Fußball-Bundesliga 2025/26 | FC Bayern München vs. VfB Stuttgart | Neuer & Urbig feiern Meisterschaft
Picha: Ulrik Pedersen/ZUMA/picture alliance

Bayern Munich ilishinda taji jingine la Bundesliga Jumapili, la 13 kwa klabu hiyo katika miaka 14, baada ya msimu uliovunja rekodi ambao bado unaweza kuwa bora zaidi.

Taji la Bundesliga ni la kwanza tu kati ya mataji matatu yanayowezekana msimu huu huku Bayern ikikabiliana na Bayer Leverkusen katika nusu fainali ya kombe la shirikisho la Ujerumani DFB Pokal Jumatano kabla ya kukabiliana na mabingwa watetezi wa Ulaya, Paris Saint-Germain katika nusu fainali ya ligi ya mabingwa Ulaya, Champions.

Taji la Bundesliga linaonekana ndani ya klabu kama shabaha ya chini kabisa kwa msimu huu na huu ni ubingwa wa 35 wa Ujerumani unaoendelea kwa rekodi kwa Bayern. Mbali na taji la kwanza mnamo 1932, lilipoamuliwa na mabingwa wa kikanda katika mashindano ya mtoano, mengine yote yalikuja baada ya kuanzishwa kwa Bundesliga mnamo 1963.

Bayern daima ina hamu ya kutangaza utawala wake wa ndani. Ushindi wa Leverkusen mnamo 2024 ulikuwa wa kipekee ambao uliisukuma Bayern kupata mataji mfululizo na inaweza kuwa mwanzo wa mfululizo mwingine mrefu.

Bayern ilirejea kutoka kwenye msiba wa mwaka 2012 - ilipopoteza fainali ya ligi ya mabingwa jijini Munich dhidi ya Chelsea, pamoja na fainali ya Bundesliga na kombe la shirikisho la Ujerumani dhidi ya Borussia Dortmund - kwa kushinda mataji matatu ya ligi ya mabingwa, Bundesliga na kombe la Ujerumani msimu uliofuata chini ya kocha wa zamani Jupp Heynckes.

Bundesliga msimu huu ni hatua ya kwanza tu huku Bayern ikifuatilia mataji matatu mengine. Huu hapa ni mtazamo wa karibu jinsi ilivyoshinda:

Magoli

Bayern ilivunja rekodi yake ya ligi kwa mabao yaliyofungwa katika msimu mmoja kwa kufunga magoli matano dhidi ya St. Pauli na kufikisha jumla ya magoli 105 wikendi iliyopita. Rekodi ya awali ilikuwa magoli 101 yaliyofungwa na timu ya Bayern ya 1971-72 ikimshirikisha Franz Beckenbauer na Gerd Müller.

Harry Kane akishangilia na watoto wake ushindi wa taji la Bundesliga wa klabu yake Bayern MunichPicha: Straubmeier/nordphoto GmbH/picture alliance

Mshambuliaji wa Uingereza Harry Kane alikuwa miongoni mwa wafungaji katika ushindi wa 4-2 dhidi ya Stuttgart Jumapili na kuongeza rekodi hiyo hadi magoli 109. Na bado kuna raundi nne zilizobaki kala msimu huu w aligi kukamilika. Kane alifikisha jumla ya magoli yake ya msimu huu hadi 50 dhidi ya Real Madrid katika nusu fainali ya ligi ya mabingwa. Sasa ni 51. Ana mabao 32 katika michezo 27 ya Bundesliga hadi sasa.

Mchezaji mpya Luis Díaz amefunga mabao 15 na Michael Olise ana mabao 12, lakini mabao ya Bayern yalitoka kote katika timu huku Leon Goretzka akifunga bao la 102 lililovunja rekodi dhidi ya St. Pauli.

Ikiwa ni pamoja na ushindi dhidi ya Stuttgart, Bayern ilifunga mabao manne au zaidi katika michezo 14 ya ligi kuanzia siku ya ufunguzi kwa ushindi wa 6-0 dhidi ya Leipzig.

Wapinzani katika ligi

Bayern tena haina mpinzani anayeweza kupinga utawala wake. Borussia Dortmund ilikaribia msimu huu lakini ilikuwa wazi kwa muda mrefu kwamba haikuweza kutoa upinzani kwa Bayern, ambayo ilimaliza dhana yoyote ya mashindano mwishoni mwa Februari kwa kushinda 3-2 huko Dortmund.

"Tuna faida ya pointi 11," Joshua Kimmich alisema wakati huo, "hatutatoa."

Dortmund ilifungua njia kwa Bayern kutwaa taji Jumapili kwa kupoteza michezo miwili mfululizo.

Hakuna hata timu moja, kuanzia Stuttgart, Leipzig au Leverkusen iliyoweza kupambana hata kuendana na Dortmund.

Kocha Vincent Kompany

Ingawa hakuwa chaguo la kwanza, kocha wa Bayern Vincent Kompany amethibitisha uteuzi uliotiwa moyo kwa timu ambayo ilikuwa ikishindwa na kutofanya vizuri chini ya kocha wa zamani Thomas Tuchel.

Kocha wa Bayern Munich, Vincent Kompany, ameiimarisha klabu hiyo ya Bavaria na kuiwezesha kushinda taji la Bundesliga.Picha: Martin Agüera/kolbert-press/picture alliance

Katika msimu wake wa pili Bayern, Kompany ameimarisha zaidi, akiwapandisha wachezaji wachanga kama Lennart Karl - ambaye anaonekana kuwa nyota - huku akibadilisha kikosi kwa uangalifu ili kuwaweka wachezaji wake wote wakihusika na kuwa na furaha huku akipunguza uwezekano wa majeraha.

Kane amekuwa na malengo ya kuvunja rekodi ya msimu ya mshambuliaji wa zamani Robert Lewandowski ya mabao 41 ya Bundesliga lakini Kompany aliamua kudhibiti muda wa kucheza wa mshambuliaji wake nyota ili kumpumzisha kwa michezo muhimu katika ligi ya mabingwa na kombe la Ujerumani.

Kompany pia alipata sifa kwa kupinga ubaguzi wa rangi baada ya José Mourinho kumlaumu nyota wa Real Madrid Vinícius Júnior kwa kuchochea matusi anayopokea, na alikaribisha uteuzi wa Marie-Louise Eta kama kocha wa kwanza mwanamke katika Bundesliga wiki iliyopita.

Kompany ameleta uelewano katika Bayern, klabu ambayo hapo awali ilijulikana kama "FC Hollywood" kwa vichwa vyote vya habari vya magazeti ya udaku ilivyoibua.

Ruka sehemu inayofuata Taarifa kuu ya DW

Taarifa kuu ya DW

Ruka sehemu inayofuata Taarifa zaidi kutoka DW