1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

John Heche ashtakiwa kwa ugaidi

5 Novemba 2025

Chama kikuu cha upinzani nchini Tanzania CHADEMA kimesema makamu mwenyekiti wake John Heche amefunguliwa mashtaka ya ugaidi, siku chache baada ya ghasia za uchaguzi kuikumba nchi hiyo.

Tanzania Daressalam | CHADEMA
Naibu mwenyekiti wa chama kikuu cha upinzani nchini Tanzania CHADEMA , John Heche akizungumza na waandishi wa habari Picha: CHADEMA

Katika chapisho kwenye mtandao wa X, jana jioni, Chadema imesema kuwa Heche ambaye alikamatwa Oktoba 22, ameshtakiwa kwa "vitendo vya ugaidi".

Kinasema polisi ilimsafirisha Heche kutoka mji mkuu Dodoma hadi eneo la pwani la Kinodoni ambako alifunguliwa mashtaka hayo.

Taarifa hiyo pia imesema naibu mwenyekiti huyo alikataa kuandika taarifa lakini atafanya hivyo mara tu baada ya kufikishwa Mahakamani.

Haijabainishwa wazi ni lini atafikishwa  mahakamani.

Mashirika ya haki yaelezea kukandamizwa kwa upinzani nchini Tanzania

Mashirika ya kutetea haki za binadamu yameelezea ukandamizaji wa kikatili dhidi ya upinzani kabla ya uchaguzi, huku viongozi wao wakifungwa jela au kuzuiwa kugombea.

Kiongozi wa chama hicho cha Chadema, Tundu Lissu, kwa sasa anakabiliwa na kesi ya uhaini ambayo inaweza kubeba hukumu ya kifo.

 

Ruka sehemu inayofuata Taarifa kuu ya DW

Taarifa kuu ya DW

Ruka sehemu inayofuata Taarifa zaidi kutoka DW