SiasaMyanmar
Jumuiya ya ASEAN haiutambui uchaguzi wa Myanmar
30 Januari 2026
Matangazo
Jumuiya hiyo yenye wanachama 11 ikiwa ni pamoja na Myanmar aidha ilikataa kuitambua serikali ya kijeshi ya taifa hilo tangu jeshi lilipochukua mamlaka kwa nguvu kutoka kwa serikali iliyochaguliwa ya Aung San Suu Kyi mnamo 2021 na kuitumbukiza nchi hiyo vitani.
Hatua hiyo iliyothibitishwa na waziri wa mambo ya Nje wa Ufilipino Theresa Lazaro inachukuliwa kuwa pigo kubwa kwa juhudi za watawala wa kijeshi wa Myanmar kutambuliwa kimataifa.
Lazaro aliyekuwa akizungumza baada ya kuongoza mkutano wa kwanza mkubwa wa mawaziri kwa mwaka huu hakueleza ikiwa jumuiya hiyo itakuja kubadilisha msimamo wake.