1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW
SiasaAsia

ASEAN yatoa wito wa kuwepo suluhisho la amani kwa mizozo

27 Julai 2024

Mawaziri wa mambo ya nje wa Jumuiya ya nchi za Kusini Mashariki mwa Asia ASEAN, wamelaani hivi leo vitendo vya ghasia dhidi ya raia katika nchi ya Myanmar inayotawaliwa na jeshi

Bendera ya Jumuiya ya ASEAN
Bendera ya Jumuiya ya ASEANPicha: picture alliance/Zoonar

Viongozi hao wamezitaka pande zote kukomesha vita na kufuata mpango wa amani ulioafikiwa. Katika taarifa ya pamoja iliyotolewa siku mbili baada ya mkutano wao huko Laos, viongozi hao walipongeza hatua za kupunguza hali ya mivutano katika Bahari ya Kusini mwa China.

Soma pia: Mawaziri wa ASEAN wakutana huko Laos

Mawaziri hao wa ASEAN wameelezea majaribio ya makombora ya Korea Kaskazini kuwa ni matukio ya kutisha huku wakihimiza kuwepo kwa suluhisho la amani katika migogoro ya Ukraine na Gaza, wakielezea wasiwasi wao juu ya hali mbaya ya kibinadamu katika maeneo hayo.

Ruka sehemu inayofuata Taarifa kuu ya DW

Taarifa kuu ya DW

Ruka sehemu inayofuata Taarifa zaidi kutoka DW