1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Juni 26: Miaka 75 ya Umoja wa Mataifa

Sekione Kitojo
26 Juni 2020

26 Juni inatimia  miaka 75 ya mkataba wa kuundwa  Umoja  wa  mataifa, uliotiwa  saini  na  mataifa  50. Hata hivyo wakati wawakilishi wakitia saini hawakuweza kuzuwia hali ya kutisha ya Vita Vikuu  vya Pili vya Dunia.

UN Sicherheitsrat  United Nations  New York  USA
Picha: picture-alliance/dpa/J. Schwenkenbecher

Ilikuwa  ni hotuba yenye  utata mwingi. Ilikuwa  hotuba yenye maneno makali dhidi ya jumuiya  ya  kimataifa. "Hali ya baadaye  ya  dunia haitakuwa upande wa utandawazi, badala  yake upande  wa wazalendo",  amesema Donald Trump katika  Umoja  wa  Mataifa  mwanzoni  mwa Septemba mwaka  uliopita. Kiongozi  huyo wa  Marekani ameiweka hali bora ya  nchi  yake  na  wananchi  wake  katika nafasi  ya  kwanza  kabisa".

Kuhusiana  na  mradi  wa  kimataifa  kwa  ajili  ya  kuhakikisha usalama duniani, hilo rais wa Marekani  hakuuma maneno, katika  jukwaa la  hadhara  kuu  ya  Umoja  wa  mataifa  mjini New York. Amejipigia debe kwamba kwa mtazamo wake  kuna hatua  kubwa  iliyopigwa,hususan katika  utwawala wake nchini Marekani, ikiwa  ni ujumbe  kwa kundi linalomuunga mkono  katika  uchaguzi.

Rais Trump bado anasisitiza sera yake ya Marekani kwanza.

Mkurugenzi Mkuu wa WHO, Tedros Adhanom GhebreyesusPicha: Getty Images/Afp/F. Coffrini

Alisisitiza kwa mara nyingine  tena kuhusu  sera yake ya Marekani kwanza.  Masuala  anayoyapa  umuhimu katika Umoja wa Mataifa  ni  ya  maamrisho. Moja ya mambo  hayo aliyaandika  katika  ukurasa  wa  twitter Disemba mwaka 2016. Muda  mfupi  kabla  ya  kuingia  madarakani  aliushutumu Umoja  wa  mataifa kuwa  ni klabu ya "watu kukutana, kupiga porojo  na  kujiburudisha tu." Mwaka  mmoja  baadaye  lakini alisababisha  mvutano  kuhusiana  na  kuhamisha  ubalozi wa Marekani  kutoka  Tel Aviv  na  kuupeleka  Jerusalem, hatua ambayo  hadhara  kuu  la  Umoja  wa  mataifa  ilishatolea maamuzi yake.

Hadi  hivi  sasa kuna hali ya mparaganyiko  wa  mahusiano, ambapo Umoja  wa  mataifa  ulifikia  makubaliano  juu  ya mabadiliko  ya  tabia  nchi, alikataa kufanyakazi na  mkataba wa  Umoja  wa  mataifa  kuhusu  wahamiaji, akapunguza mchango  wa  Marekani  katika  ujumbe wa  kulinda  amani na kujitoa  kutoka  katika  shirika  la  Sayansi  na  Utamaduni UNESCO pamoja  na  baraza la  haki  za  binadamu  la Umoja  wa  mataifa.

Malalamiko ya mapungufu kwa WHO

Pia Trump  alililalamikia  shirika  la  afya  ulimwenguni WHO kuwa  linamapungufu.  Kutokana  na  utendaji  wa  shirika hilo  kabla  ya  mzozo  wa  virusi vya  corona  kusambaa, alilishambulia mwezi Mei, kwamba  halitaki  kufanya  mageuzi na  kwamba  ni shirika  hilo  limekuwa  kikaragosi  wa  China. Ametishia  kuvunja  uhusiano  na  shirika  hilo. Lengo kuu  la  Umoja  wa  mataifa ni  pamoja  na  kufanyakazi kwa  pamoja  na  jamii ya kimataifa. Ili  kupatikana amani duniani ni lazima  kuachana  na hali ya  kuthamini  utaifa.

Soma zaidi:Ujerumani: Tutaisaidia kifedha WHO

Kwa hiyo  basi  kulikuwa  na  haja  ya  kupatikana  utaratibu wa  mkataba  utakaokuwa  na  ujumuisho wa  jumla duniani, ambao ni Mkataba  wa  Umoja  wa  mataifa. Wakati wawakilishi wa  mataifa  50 wakitia  saini  mkataba  huo  wa kuundwa  kwa  Umoja  wa  mataifa  tarehe 26, Juni 1945 mjini San Francisco , wawakilishi  hao  walikuwa wamo  katika athari  za  vita  viwili  vikuu  vya  dunia.

Ruka sehemu inayofuata Taarifa kuu ya DW

Taarifa kuu ya DW

Ruka sehemu inayofuata Taarifa zaidi kutoka DW